Kiungo mpya wa Yanga, Papy Kabamba Tshishimbi.
Fasta baada ya mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Yanga ikafungwa kwa penalti 5-4, kiungo huyo alikabidhiwa gari likiwa na dereva wake kwa matumizi binafsi. Yanga imeamua kumpa Tshishimbi raia wa DR Congo gari hilo aina ya Ford Ranger lililo katika muundo wa ‘Double Cabin’ lenye rangi ya chungwa na jana alionekana nalo mazoezini Uwanja wa Uhuru.
Papy Kabamba Tshishimbi akiingia katika gari alilopewa aina ya Ford Ranger lililo katika muundo wa ‘Double Cabin’ .
Gari analotumia Tshishimbi kama ukilitaka jipya lake utalazimika kutoa si chini ya Sh milioni 100, kwa kuwa ndiyo bei yake kwani mengi yake ni mapya na yanatoka kiwandani Afrika Kusini. Tshishimbi amesajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Klabu ya Mbabane Swallows ya Swaziland na baada ya kucheza mechi mbili tu, amejizolea umaarufu mkubwa nchini.
Ford Ranger lililo katika muundo wa ‘Double Cabin’.
“Huyu kiungo anakaa Mbezi sasa bila gari anaweza kupata tabu ya kuwahi mazoezini ukizingatia ni mgeni hapa nchini, gari hili atalitumia katika muda huu na yeye analitumia tu.” Alipotafutwa Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten, alisema: “Hilo gari Tshishimbi analitumia tu kwa kuwahi na kutoka mazoezini kwenda kwake, haimaanishi kama klabu imempa moja kwa moja.”
Akiendelea kukagua garui lake hilo.
Source : Champion




No comments:
Post a Comment