Jose Mourinho akubali yaishe kuhusu kesi yake ya kodi na kutoa kiasi hiki - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Friday 3 November 2017

Jose Mourinho akubali yaishe kuhusu kesi yake ya kodi na kutoa kiasi hiki

Zikiwa zimebaki siku mbili kuelekea mpambano kati ya Manchester United zidi ya Chelsea, hii leo kocha wa Manchester United Jose Mourinho alikuwa nchini Hispania kusikiliza kesi yake ya kuhusu ukwepaji kodi
Mourinho asubuhi ya leo saa nne tayari alikuwa amewasili katika mahakama mjini Madrid katika eneo liitwalo Puzuelo Del Alacron tayari kusikiliza hukumu ya kosa hilo alilotenda wakiwa akiwa Real Madrid.
Baada ya muda kesi hiyo kuisha Mourinho alitoka nje ya mahakama ambako kulikuwa na waandishi wa habari na kuwaambia kuwa amekubali kulipa kiasi hicho anachodaiwa ambapo ni €3.3m.
Kesi ya Jose Mourinho ilikuwepo tangu mwezi wa sita mwaka huu akidaiwa kwamba alikuwa akikwepa baadhi ya masuala ya kodi katika kipindi cha mwaka 2011 hadi 2013.
Wakati kesi ya Mourinho inaanza alikana mashtaka na kusema aliondoka Hispania akiwa msafi kuhusu kodi na wakili wake aitwaye Gestifute Media akizishangaa mamlaka za kodi za Hispania akidai Mourinho alilipa zaidi ya £23m ya kodi akiwa Hispania.
Hii sio mara ya kwanza kwa wanasoka katika ligi kuu La Liga kukumbwa na kashfa za ukwepaji kodi kwani Angel Di Maria, Lioneil Messi, Cristiano Ronaldo na Javier Mascherano wameshakumbwa na kesi za namna hii.
Baada ya kesi hiyo sasa Mourinho anapakia ndege kurudi nchini Uingereza kuiandaa timu kwa ajili ya pambano kubwa na gumu siku ya Jumapili zidi ya Chelsea

No comments:

Post a Comment