Zikiwa zimebaki siku mbili kuelekea mpambano kati ya
Manchester United zidi ya Chelsea, hii leo kocha wa Manchester United
Jose Mourinho alikuwa nchini Hispania kusikiliza kesi yake ya kuhusu
ukwepaji kodi
Mourinho asubuhi ya leo saa nne tayari alikuwa amewasili katika
mahakama mjini Madrid katika eneo liitwalo Puzuelo Del Alacron tayari
kusikiliza hukumu ya kosa hilo alilotenda wakiwa akiwa Real Madrid.
Baada
ya muda kesi hiyo kuisha Mourinho alitoka nje ya mahakama ambako
kulikuwa na waandishi wa habari na kuwaambia kuwa amekubali kulipa kiasi
hicho anachodaiwa ambapo ni €3.3m.
Kesi ya Jose Mourinho ilikuwepo tangu mwezi wa sita mwaka huu
akidaiwa kwamba alikuwa akikwepa baadhi ya masuala ya kodi katika
kipindi cha mwaka 2011 hadi 2013.
Wakati
kesi ya Mourinho inaanza alikana mashtaka na kusema aliondoka Hispania
akiwa msafi kuhusu kodi na wakili wake aitwaye Gestifute Media
akizishangaa mamlaka za kodi za Hispania akidai Mourinho alilipa zaidi
ya £23m ya kodi akiwa Hispania.
Hii sio mara ya kwanza kwa wanasoka katika ligi kuu La Liga kukumbwa
na kashfa za ukwepaji kodi kwani Angel Di Maria, Lioneil Messi,
Cristiano Ronaldo na Javier Mascherano wameshakumbwa na kesi za namna
hii.
Baada
ya kesi hiyo sasa Mourinho anapakia ndege kurudi nchini Uingereza
kuiandaa timu kwa ajili ya pambano kubwa na gumu siku ya Jumapili zidi
ya Chelsea
Friday 3 November 2017
Jose Mourinho akubali yaishe kuhusu kesi yake ya kodi na kutoa kiasi hiki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
olger tz ni blog ya kuhusu habari zote za ulimwenguni hapa utaelimika utaburudika na kunufaika na mambo mbalimbali ! ungana nasi kwa habari za kitaifa,kimataifa ,michezo bila ya kusahau habari za wasanii ,visa na mikasa na kadharika!!
No comments:
Post a Comment