Watu wanne washikiliwana Polisi kwa kosa la kumzomea mke wa Raisi - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Saturday 11 November 2017

Watu wanne washikiliwana Polisi kwa kosa la kumzomea mke wa Raisi


Image result for grace mugabe picture 
Watu wanne wamekamatwa nchini Zimbabwe wakituhumiwa kumzomea mke wa rais wa nchi hiyo Grace Mugabe wakati akihutubia mkutano wa hadhara siku ya jumamosi iliyopita.

Gazeti linalomilikiwa na Serikali la The Herald limeripoti kwamba watuhumiwa hao wanakabiliwa na mashitaka ya kupuuza mamlaka ya rais.

Kuzomea huko kuliibuka kati ya makundi mawili ndani ya chama tawala cha Zanu-PF yanayopambana juu ya nani atakuwa mrithi wa rais Robert Mugabe ambapo kuna kundi linalimuunga mkono mke wa rais Grace Mugabe na lile linalomuunga mkono Makamu wa rais aliyefukuzwa Emmerson Mnangagwa.

Imedaiwa kwamba watu hao waliokamatwa ni wafuasi wa aliyekuwa Makamu wa Rais
Watu hao walikamatwa mara baada ya mkutano huo uliofanyika mjini Bulawayo,watuhumiwa hao inasemekana ni aliyefukuzwa Emmerson Mnangagwa .

Watuhumiwa hao waliokamatwa ni wanaume watatu na mwanamke mmoja wako nje kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment