Magufuli aagiza kusimamishwa kazi kwa naibu kamishana wa uhamiaji - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Friday 28 July 2017

Magufuli aagiza kusimamishwa kazi kwa naibu kamishana wa uhamiaji


Magufuli aagiza kusimamishwa kazi kwa naibu kamishana wa uhamiaji
Rais John Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi kwa naibu kamishna wa uhamiaji kwa tuhuma za kuingiza nchini humo raia 50 wa Somalia na kuwapa vibali vya kuishi.
Kupitia waziri mkuu Kassim Majaliwa kiongozi huyo ametaka kusimamishwa kazi mara moja kwa bi Grace Hokororo na kuundwa kwa tume itakayochunguza utoaji wa vibali vya uraia nchini humo.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumaliza kikao na Makamishna wa uhamiaji kilichofanyika katika makao makuu ya uhamiaji jijini Dar es salaam.
Tayari Majaliwa amemuagiza waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba kubuni tume hiyo ya uchunguzi.
Amesema kuwa haiwezekani raia wa kigeni kuingizwa nchini humo na baadaye kupewa vibali vya kuishi bila ya kufanyiwa uchunguzi wa kina


source:bbc

No comments:

Post a Comment