Muigizaji Wema Sepetu.
Siku chache baada ya picha za muigizaji Wema Sepetu na bwana’ke mpya aitwaye Bakari Kila akiwa bafuni kuvuja, mrembo huyo amedaiwa kulianzisha kumsaka ‘snichi’ aliyezivujisha.
Wema Sepetu na bwana’ke mpya aitwaye Bakari Kila wakiwa bafuni.
Picha za Wema na Kila wakiwa bafuni zilivuja wiki kadhaa zilizopita katika gazeti ndugu na hili la Ijumaa Wikienda ambapo kwenye picha hizo, Wema alionekana akiwa amevalia kanga moja huku akimpiga busu motomoto Kila.
Mara baada ya ubuyu huo kuanikwa gazetini, chanzo makini kimeeleza kuwa, kuliibuka tafrani la aina yake wakati Wema alipokuwa akihaha kumtafuta mchawi.
“Unajua Madam (Wema) ni kama alichanganyikiwa. Alishindwa kung’amua hasa nani ni mdudu mtu ambaye alivujisha picha hizo. Mazingira ya picha hizo walipiga wakiwa wawili, yeye na mpenzi wake tena kimahaba zaidi.
Wema Sepetu akiwa katika pozi.
Wakifanya yao.
“Unajua hizi mpya ziko romantic sana. Walikuwa nazo wao wawili tu, yeye na bwana wake sasa anajiuliza ni nani amezitoa hadi zikawafikia Global?,” kilisema chanzo hicho.
Kuonesha kwamba amekerwa na kuvuja kwa picha hizo, Wema alionesha masikitiko yake kupitia kwenye mtandao wa Instagram ambapo alilalamika kuwa mtu aliyemuamini ndiye aliyevujisha hizo picha.
Licha ya Amani kuona povu la Wema mitandaoni akimlaumu aliyevujisha picha hizo (si ambaye amezivujisha Global), lilijaribu kumvutia waya Wema ili kumsikia kama ana lolote kuhusiana na picha hizo, simu yake iliita bila kupokelewa
Credit goes to Global publisher
No comments:
Post a Comment