Mchuano mkali wa ndondi kati ya Conor McGregor na mwanandondi Floyd
Mayweather Jnr umemalizika huko Las Vegas, Nevada nchini Marekani, baada
ya kuchelewa kuanza kwa muda wa saa moja hivi.
Floyd Mayweather Jnr ameibuka mshindi katika mchuano huo.
Maelfu
ya watu wamefika katika mji wa Las Vegas katika jimbo la Nevada nchini
Marekani, kutizama mchuano huo mkali wa ndondi, unaofanyika leo Jumapili hiiMasumbwi hayo yalikuwa ya raundi kumi. Awali wachanganuzi walisema
kuwa Floyd Mayweather Jnr alikuwa ameanza kulemewa katika raundi tatu za
mwanzo na mpinzani wake, kabla ya kujizoazoa na kuanza kumrushia
makonde mazito mazito Conor McGregor, ambaye alionekana kulemewa hasa
kuanzia raundi ya saba.
Alishindwa kuhimili makonde mazito ya Maywheather na kushindwa kumaliza raundi ya 10,Tayari McGregor ambaye amechana chale mwilini, ni bingwa wa taji la
Ultimate Fighting- mchezo ambao mwanandondi anatumia mbinu zote za
upiganaji, akitumia makonde na mateke.Lakini nyota huyo wa miaka 29, hawajawahi kushiriki mchuano wa makonde
ya kulipwa- Huku May-weather menye umri wa miaka 40 akitajwa kuwa
mpinzani wake hatari zaidi katika masumbwi.Mayweather, anapigiwa upatu wa kushinda mchuano huo, huku akiahidiwa
dola milioni 100, ilihali mpinzani wake McGregor, akiahidiwa Dola
milioni 30.
Dola milioni 600 zinatazamiwa kupatikana kutokana na
mauzo ya moja kwa moja ya tiketi ya kutizama makabiliano hayo ya ndondi.
Ambayo pia inatizamwa na mamilioni ya watu moja kwa moja kwenye Runinga
huku wengine wengi wakifuatilia katika mitandao.
hapa floyd mayweather akikumbatiana na McGregor ambae amekubali kipigo na kumfanya floyd kuibuka mshindi
Saturday 26 August 2017
Home
michezo
Floyd Mayweather amchakaza vibaya baya hasimu wake Conor McGregor katika mpambano huko, Las Vegas, Nevada
Floyd Mayweather amchakaza vibaya baya hasimu wake Conor McGregor katika mpambano huko, Las Vegas, Nevada
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
olger tz ni blog ya kuhusu habari zote za ulimwenguni hapa utaelimika utaburudika na kunufaika na mambo mbalimbali ! ungana nasi kwa habari za kitaifa,kimataifa ,michezo bila ya kusahau habari za wasanii ,visa na mikasa na kadharika!!
No comments:
Post a Comment