Kyler Walker analipwa mshahara wa pound 130000 kwa wiki ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 370 wakati John Stones analipwa mshahara wa pound 100000 ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 288, Stones na Walker leo wameonekana wakitembelea gari yenye gharama ndogo.
Licha ya mastaa hao kuwa na uwezo wa kumiliki gari aina yoyote ambayo mioyo yao itapenda kutumia, John Stones alionekana akimuendesha Kyler Walker katika gari hiyo na kuelekea mazoezini wakiwa wanafuraha, kitendo hicho kimewafanya waingie kwenye headlines kwa sababu haijazoeleka kuona mastaa kama wao kutembelea gari za bei ndogo.
Kwa pamoja Walker na Stones wanalipwa pound 230,000/= ambazo ni zaidi ya milioni 650 za kitanzania, mshahara ambao kila mmoja anaweza kununua aina yoyote ya gari, sema wameamua kutembelea gari ya kawaida.
No comments:
Post a Comment