Chadema: Taarifa Ya Awali Kuhusu Shambulio La Kupigwa Risasi Tundu Lissu - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Thursday 7 September 2017

Chadema: Taarifa Ya Awali Kuhusu Shambulio La Kupigwa Risasi Tundu Lissu

Image result for Tundu Antipas Lissu picha 
Mwanasheria Mkuu wa Chama ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Antipus Lissu.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kupigwa risasi Mwanasheria Mkuu wa Chama ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Antipus Lissu baada ya kikao cha Bunge mchana wa leo.
Shambulio hilo limetokea majira ya mchana nyumbani kwake Area D Dodoma na kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika Hosiptali ya Mkoa wa Dodoma.
CHADEMA tunalaani vikali kitendo hicho, na tunafuatilia kwa karibu hali yake.
Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.
Imetolewa na Kurugenzi ya Uenezi, Mawasiliano na Mahusiano ya Nje.
CHADEMA MAKAO MAKUU
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment