Kesi ya Manji Tarehe ya hukumu Yapangwa - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Wednesday 27 September 2017

Kesi ya Manji Tarehe ya hukumu Yapangwa


Manji na hakimu wake.
 
MAHAKAMA ya Hakimu ya Mkazi Kisutu, imepanga Oktoba 6, mwaka huu kutoa  hukumu katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Yusuf Manji (41).
Uamuzi huo umetolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha, baada ya wakili wa utetezi Hajra Mungula kusema kuwa ameshafunga ushahidi wa mashahidi saba.
Mashahidi watatu wa upande wa mashtaka wametoa ushahidi wao dhidi ya mshtakiwa Daktari Mfawidhi wa Gereza la Keko, Inspekta Eliud Mwakawanga ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi maisha ya mfanyabiashara Yusufu Manji yalivyo kuwa gerezani kwamba alikuwa akitumia vidonge kati ya 25 mpaka 30 kwasiku.
Alieleza kwamba  walikuwa wakimpatia dawa hizo alipokuwa akisikia maumivu hasa ya mgongo na kwamba kuna kipindi alikuwa anaamka akiwa na hali ya kutetemeka au kuchanganyikiwa.
Alisema kuwa Julai 6, 2017 walimpokea Manjia kitokea Hospitali ya Muhimbili Kitengo cha Moyo cha JKCI ambapo waliambiwa ni mshtakiwa lakini ni mgonjwa.
“Nilienda kumuona, tukazungumza naye na tulikaa naye gerezani hadi alipokuja kuachiwa,”

No comments:

Post a Comment