Polisi mjini Dar es Salaam nchini Tanzania mapema siku ya Jumamosi wamesema kuwa wanaendelea kuchunguza kiwango cha mlipuko uliokumba kampuni moja maarufu ya mawakili katika shambulio la usiku.
''Sisi maafisa wa polisi tunachunguza swala hili.Tayari tumelitenga eneo hilo'',alisema kamanda Mkondya akiongezea: uchunguzi utakapokamilika tutakuwa na uwezo wa kusema ni nini kilichosababisha mlipuko huo.
Amesema kwamba kufikia sasa hakuna mtu aliyetiwa mbaroni kufuatia kisa hicho.
Shahidi mmoja wa kampuni hiyo amesema kuwa afisi hizo ziliharibiwa lakini hakuna kitukilichoibwa.''Wacha tuwaachie polisi wafanye uchunguzi wao'' , alisema wakili Magai.
Jumba la IMMMA lililopo katika eneo la Upanga katika barabara ya Umoja wa Mataifa lilikumbwa na mlipuko mwendo wa saa nane alfajiri.
Fatma Karume wakili maarufu na mwana wa aliyekuwa rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume ni mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo
No comments:
Post a Comment