aliyoyasema Young Dee kwa Dogo Janja na Young Killer - Olgertz
TANGAZA NASI HAPA

Breaking News

Home Top Ad

TANGAZA NASI HAPA

Friday 22 September 2017

aliyoyasema Young Dee kwa Dogo Janja na Young Killer


 Image result for Young Dee.

Msanii wa HipHop nchini, Young Dee.
MSANII wa HipHop nchini,   Young Dee,  anayetamba na ngoma yake mpya ya Utani Utani ametoa povu juu ya kauli ya Young Killer, pale Young Killer  aliposema kuwa Young D na Dogo Janja hata wakiingia studio wote halafu wafanye ngoma ya pamoja,  na yeye Young Killer aingie studio afanye ngoma yake peke yake,  bado hawatamfikia hata wafanyeje.

Pia Young Killer alisema kuwa mashabiki wasimfananishe na hao watu kwani haendani nao hata kidogo.
Alichofunguka Young Dee kuhusu kauli ya Young Killer kusema hawamuwezi, ni kuwa Young Killer na Dogo Janja  ni vifaranga vyake,  kwa hiyo hawamuwezi hata kidogo.

Alipoulizwa kama ikitokea shoo ya pamoja  baina ya yeye, Dogo Janja na Young Killer, alisema uwezo wake ni mkubwa sana, hawezi kufanya shoo kwenye jukwaa moja nao.

”Inategemea hiyo shoo imeandaliwa kwa aina gani kwa sababu mimi sasa hivi nimekua, kwa hiyo siwezi kufanya shoo ya pamoja na hao vifaranga vyangu.  Sidhani kama itakuwa shoo nzuri kwa mashabiki zangu kwa sababu  mimi nikiwa jukwani ni mtu mkubwa sana.  Ukiwakusanya wote hao labda ndiyo unaweza kupata nusu ya Young Dee,” alisema Young Dee

Siku zote hamna msanii ambaye anakubali kufunikwa lakini hii ya hawa vijana wanaofanya muziki wa HipHop imekuwa balaa pale kila mtu anapojiona yupo juu ya mwenziye, lakini wote ni wakali wa HipHop kutoka Tanzania kwenye kisiwa cha burudani.

No comments:

Post a Comment